Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Jenerali Nyamvumba, mkuu mpya wa majeshi Rwanda

Rais Paul Kagame wa Rwanda amefanya mabadiliko kwenye safu za uongozi wa jeshi na kumteua Jenerali Patrick Nyamvumba kuwa mkuu mpya wa majeshi ya nchi hiyo. Jenerali Nyamvumba amechukua nafasi ya Jenerali Charles Kayonga aliyeshikilia nafasi hiyo tangu mwaka 2002. Mkuu mpya wa majeshi ya Rwanda alikuwa kamanda wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa UNAMID katika jimbo la Darfur nchini Sudan tangu mwaka 2009. 
Mabadiliko hayo pia yamepelekea kubuniwa wadhifa mpya wa Mkaguzi Mkuu wa jeshi uliopewa Brigedia Jenerali Jack Nziza baada ya kupandishwa cheo na kuwa Meja Jenerali. Nziza amekuwa akihudumu kama mkurugenzi mkuu katika wizara ya ulinzi. Pia mkuu wa zamani wa idara ya upelelezi wa nje kanali Dany Munyuza ameteuliwa kuwa naibu kamishna mkuu wa polisi ya Rwanda. Rais Kagame amesema mabadiliko hayo yanalenga kuimarisha huduma kwa wananchi na vilevile kuinua hali ya usalama nchini.

No comments: