Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Viongozi wa Misri walaani mauaji ya Mashia

Rais Muhammad Mursi wa Misri na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Hesham Qandil wamelaani mauaji ya Waislamu wanne wa Kishia katika eneo la Giza yaliyofanywa hapo jana. Taarifa iliyotolewa na ofisi ya Rais imelaani mauaji hayo na kueleza kuwa, serikali haitomvumilia mtu yeyote anayehatarisha usalama wa taifa na mshikamano wa wananchi wa Misri. Kwa upande wake Hisham Qandil amesema kwamba tukio hilo la kinyama ni kinyume na mafundisho ya diniya Kiislamu. 
Hapo jana genge la watu waliongozwa na viongozi wa kisalafi katika kijiji cha Zawyat Abu Musalama, walishambulia eneo lenye wakaazi wa Kiislamu wa Kishia na kuwaua watu wanne akiwemo shakhia mkubwa wa madhehebu hiyo.
Mahakama ya Misri imetoa waranti wa kukamatwa watu 15 waliohusika na mauaji hayo huku uchunguzi ukiendelea. Haya yanajiri huku baadhi ya makundi ya Misri yakimlaumu Rais Mursi kuwa, huenda matamshi yake ya ubaguzi wa kidini aliyoyatoa hivi karibuni ndiyo yamesababisha kuuawa Mashia hao katika eneo la Giza.

No comments: