Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Mwana wa Museveni akanusha kumrithi baba yake

Mwana wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema kwamba, hana mpango wa kumrithi baba yake, na hivyo kukanusha tuhuma ambazo amekuwa akielekezewa na wapinzani kwa wiki kadhaa sasa kwamba anajitayarisha kuchukua madaraka ya nchi hiyo.
Muhoozi Kainerugaba ambaye pia ni kamanda wa vikosi maalumu amesema kuwa, Uganda sio nchi ya kifalme ambapo uongozi hurithiwa na mtoto kutoka kwa baba yake.
Kijana huyo mwenye miaka 39 amesema, Waganda ndio wanaoamua Uganda iongozwe na nani, na kwamba sio mtu mmoja kama baadhi wanavyoamini.
Mwezi uliopita polisi ya Uganda ilifunga kwa siku 10 magazeti mawili binafsi pamoja na vituo viwili vya redio nchini humo baada ya kuripoti mjadala wa baadhi ya majenerali wa jeshi waliodai kwamba Rais Museveni anamtayarisha mwanaye huyo kuchukua uongozi wa nchi baada yake.

No comments: