Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Jeshi la Lebanon lasisitiza kuzima fujo kusini mwa nchi

Jeshi la Lebanon limetangaza kuwa, litaendelea na oparesheni zake kwa ajili ya kuhitimisha uasi ulioanzishwa na sheikh wa kisalafi Ahmad al Assir na wafuasi wake waliofurutu ada, na kusababisha watu kadhaa kuuawa. Katika taarifa yake jeshi la Lebanon limetangaza leo kuwa, sheikh Ahmad  Al Assir ndiye msababishaji mkuu wa machafuko na mapigano huko Sweida na kumtaka yeye na wafuasi wake kueka silaha chini na kuacha kukabiliana na jeshi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mapigano makali bado yanaendelea kati ya vikosi vya jeshi na wanamgambo wanaofungamana na Ahmad al Assir sheikh mfitini wa kisalafi kwenye mji wa Sweida kusini mwa Lebanon. Katika mapigano hayo watu wasiopungua 52 wameuawa wakiwemo wanajeshi wa serikali.
Mapigano hayo yalianza hapo jana katika mji huo baada ya wafusi wa sheikh huyo wa kisalafi waliofurutu ada kushambulia wanajeshi na kuwaua watu 10 wakiwemo askari wawili. Rais Michael Suleiman wa Lebanon amelitaka jeshi kukabiliana vilivyo na Sheikh al Assir na wafuasi wake ili kurejesha amani na utulivu kwenye mji wa Sweida.

No comments: