Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 22, 2013

Uchaguzi wa rais wa Iran ni ushindi mkubwa

Khatibu wa sala ya Ijumaa hapa mjini Tehran amesema kuwa duru ya 11 ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni ushindi adhimu kwa taifa la Iran katika chimbuko la hamasa ya kisiasa. Ayatullah Muhammad Ali Muvahidi Kermani Khatibu wa sala ya Ijumaa ya mjini Tehran amesifu na kuwashukuru wananchi  wa Iran ya Kiislamu kwa kushiriki kwa wingi katika hamasa ya kisiasa na kueleza kuwa hamasa hiyo ilikuwa itikio kwa wito wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa ajili ya kushiriki katika uchaguzi huo wa rais.
Ayatullah Muvahidi Kermani amesisitiza kuwa hamasa ya kisiasa ya Juni 14 2013 kwa mara nyingine tena imelipa heshima na fakhari taifa la Iran na kupelekea kushindwa maadui wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Khatibu wa sala ya Ijumaa ya Tehran pia amempongeza Sheikh Dakta Hassan Ruhani Rais mteule wa Iran na kumtaja kuwa kiongozi shupavu, mfuasi wa utawala wa faqihi na mwenye rekodi nzuri kabla na baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu. 

No comments: