Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 22, 2013

Al-Bashir aonya juu ya mapigano ya kikabila

Rais Omar Hasan al Bashir wa Sudan ameonya juu ya hatari ya mapigano ya kikabila ambayo yamekuwa yakitokea katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo. Al Bashir ameyasema hayo leo katika kikao cha Baraza la Ushauri la Kongresi ya Kitaifa na kuongeza kuwa, mapigano hayo ambayo yamekuwa yakijiri katika baadhi ya maeneo ya nchi yake, ni hatari kubwa  kwa taifa la Sudan na kwamba, serikali yake inakabiliwa na changamoto kubwa katika kuzuia hali hiyo. Amesema kuwa, baadhi ya watu katika baadhi ya makabila, wamekuwa wakizusha na kuchochea chokochoko za mapigano hayo ya kikabila.
Kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa, katika miezi ya hivi karibuni, mapigano ya kikabila na kikaumu katika maeneo tofauti ya jimbo la Darfur yameshtadi baada ya kupita kupindi kirefu cha utulivu. Wiki iliyopita watu 40 waliripotiwa kuuawa katika mapigano ya kikabila jimboni humo. Hii ni katika hali ambayo mwaka 2003, eneo hilo lilishuhudia mapigano makali yaliyopelekea idadi kubwa ya watu kuuawa na kujeruhiwa huku maelfu ya wengine wakilazimika kuwa wakimbizi.

No comments: