Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Serikali ya Kenya kutumia nguvu kurudisha amani

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kuwa, serikali yake iko tayari kutumia nguvu kurudisha amani na utulivu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Rais Kenyatta amewataka viongozi wa kikabila katika maeneo ya Wajir, Mandera na Garissa kuyashawishi makundi yenye silaha kusalimisha silaha hizo kwa serikali mara moja la sivyo ataliamuru jeshi na vyombo vingine vya usalama kutumia nguvu. Kiongozi huyo ametoa onyo hilo katika hali ambayo, maeneo hayo ya kaskazini mashariki mwa nchi yamekuwa yakishuhudia mauaji ya kutisha dhidi ya raia na maafisa wa usalama.
Maeneo hayo yanahesabiwa kuwa hatari mno kwani yako karibu na mpaka wa Somalia. Huku hayo yakijiri, Shirika la kimataifa la kufuatilia migogoro ICG limetoa orodha ya nchi zinazofanya vyema na zile zinazoburuza mkia katika masuala ya amani, uthabiti na demokrasia. Somalia imeorodheshwa ya kwanza kama nchi hatari zaidi kiusalama duniani. Kenya licha ya kuendesha uchaguzi wa amani mwezi Machi mwaka huu, imetajwa kuwa miongoni mwa nchi 20 ambazo zimeshindwa kulinda demokrasia na haki za binadamu. Uganda inashikilia nafasi ya 22. Tanzania imewekwa katika nafasi ya 65 na kutajwa kuwa salama zaidi kushinda China na Utawala haramu wa Israel.

No comments: