Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

Mapigano mapya ya kikabila yauwa watu 11 Darfur

Wimbi jipya la mapigano mapya kati ya makabila hasimu yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 11 huko Darfur, magharibi mwa Sudan. Watu walioshuhudia wamesema kuwa mapigano makali yaliibuka juzi katika eneo la Edd al Fursan umbali w akilomita 100 kusini magharibi mwa  Nyala makao makuu ya jimbo la Darfur Kusini.
Watu hao waliuliwa baada ya watu wa kabila la Beni Halba kuvishambulia vijiji vya wenzao wa kabila Gimir katika eneo hilo.
Kiongozi wa kabila la Gimir ameeleza kuwa watu wa kabila la Beni Halba walivamia na kushambulia vijiji vyao wakiwa na magari, pikipiki , farasi, ngamia na silaha nzito na kwamba wenzao watano wameuawa katika mapigano.
Naye mkuu wa kabila la Beni Halba amesema kuwa, watu sita wa kabila lao wameuawa kwenye mapigano hayo. Amesema wanapigana ili kulinda ardhi yao.

No comments: