Mdahalo wa tatu wa wagombea urais nchini Iran, umeakisiwa sana na vyombo
mbalimbali vya nchi za nje. Shirika la Habari la Ufaransa, limeripoti
kuwa, katika mdahalo mkali wa tatu na wa mwisho wa televisheni, wagombea
wa urais katika uchaguzi wa wiki ijayo, wamekosoa siasa za baadhi ya
wawakilishi wa mazungumzo ya nyuklia kati ya Tehran na madola yenye
nguvu duniani. Shirika hilo la habari limeutaja mdahalo huo, kuwa
uliojikita zaidi kuhusiana na siasa za mambo ya nje ya Iran huku maudhui
kuu ikiwa ni kadhia ya nyuklia. Kwa upande wake Shirika la Habari la Associated Press
limetangaza kuwa, wagombea wanane wa uchaguzi wa rais nchini Iran,
walitofautiana kuhusiana na namna ya kuendesha mazungumzo ya nyuklia
kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kundi la 5+1.
Nayo televisheni ya
habari ya Bloomberg imetangaza kuwa, mdahalo wa siku ya Ijumaa kati ya
wagombea urais nchini Iran, ulijikita katika masuala ambayo
hayakutarajiwa kabisa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment