Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

Jumatano, Juni 26, 2013

Leo ni Jumatano tarehe 17 Shaaban 1434 Hijria inayosadifiana na tarehe 26 Juni 2013.
Siku kama ya leo miaka 53 iliyopita Madagascar ilipata uhuru kutoka kwa mkoloni Mfaransa. Kuanzia katikati mwa karne ya 18, Uingereza na Ufaransa zilianzisha ushindani wa kuidhibiti nchi hiyo ya Kiafrika. suala hilo lilipelekea kudhibitiwa mara kadhaa kisiwa hicho na nchi mbili hizo na hatimaye mwishoni mwa karne ya 19, Ufaransa ikafanikiwa kuidhibiti kikamilifu Madagascar.
Hata hivyo wananchi wa Madagascar waliendesha mapambano mengi ya ukombozi dhidi ya wakoloni wa Kifaransa, miongoni mwake ni yale ya mwaka 1947 ambapo karibu watu elfu 80 waliuawa.
Miaka 68 iliyopita sawa na tarehe 26 Juni 1945, mkutano wa kimataifa wa San Francisco ulimaliza shughuli zake katika mji unaojulikana kwa jina hilo huko Marekani kwa kupasishwa hati ya Umoja wa Mataifa. Mkutano huo ambao ulikuwa wa kwanza wa kimataifa kufanyika baada ya Vita vya Pili vya Dunia, ulihudhuriwa na wawakilishi wa nchi 50 waitifaki katika vita hivyo.
Na siku kama ya leo miaka 759 iliyopita alizaliwa Marco Polo mfanyabiashara na mtalii mashuhuri wa Kiitalia huko katika mji wa Venice. Baba na mjomba wa Marco Polo walikuwa miongoni mwa watalii mashuhuri wa Italia ambao walifanya safari huko Uchina ya Kaskazini, Mongolia, Turkistan ya Mashariki na Iran, nchi ambazo wakati huo zilikuwa chini ya utawala wa warithi wa Chengiz. Akiwa kijana, Marco Polo alielekea Uchina pamoja na baba yake na kuanza kufanya biashara nchini humo kwenye visiwa vya mashariki mwa bara la Asia kwa muda fulani.

No comments: