Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

Bunge la Libya lamchagua kiongozi mpya

Bunge la Libya limemchagua Nouri Abusahmain kuwa spika mpya kufuatia kujiuzulu mtangulizi wake, Mohammed Magarief. Abusahmain ambaye anatoka katika kabila la wachache alijipatia kura 96 huku mpinzani wake wa karibu, Al-Sharif al-Wafi akijipatia kura 80. Magarief alijiuzulu kufuatia kupitishwa sheria inayopinga watu waliohudumu katika serikali ya Muammar Gaddafi kushikilia nyadhifa zozote za umma. Ingawa Magarief aliwahi kuhudumu katika serikali ya Gaddafi, alikuwa na mchango mkubwa katika mapinduzi yaliyopelekea kupinduliwa dikteta huyo mwaka 2011.
Sheria hiyo mpya inasisitiza kuwa, kila aliyehudumu chini ya Gaddafi hafai kushikilia wadhifa wowote hata kama alimpinga dikteta huyo wakati wa harakati za mapinduzi.  Spika mya ataongoza kamati itakayotayarisha rasimu ya katiba mpya ambayo baada ya kukamilika, itapigiwa kura na wananchi. Katiba mpya itatoa fursa ya kufanyika uchaguzi wa rais na kuirudisha Libya katika hali ya kawaida kisiasa.

No comments: