Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 22, 2013

Hamdallah akataa ombi la kubadili msimamo wake

Waziri Mkuu mpya wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina aliyejiuzulu, Rami Hamdallah, amepinga ombi la kumtaka abadili msimamo wake wa kujiuzulu wadhifa huo. Hii ni katika hali ambayo mazungumzo ya leo kati ya waziri mkuu huyo aliyetangaza kung’atuka madarakani baada ya kuhudumu katika nafasi hiyo kwa muda wa chini ya wiki mbili, na Tayeb Abdul Rahim Mshauri Mkuu wa Mahmoud Abbas Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina na Majid Faraj Mkuu wa Idara ya Kiintelijensia ya Mamlaka hiyo, yamemalizika bila kufikiwa natija yoyote.
Duru za habari zinaarifu kuwa, katika mazungumzo hayo Tayeb Abdul Rahim na Majid Faraj walikuwa wakimtaka Hamdallah abadili msimamo wake wa kujiuzulu na kumuomba aendelee katika nafasi hiyo. Tofauti kati ya waziri mkuu huyo na manaibu wake, zinatajwa kuwa chanzo cha kujiuzulu kwake. Rami Hamdallah aliteuliwa kuchukua nafasi ya mtangulizi wake, Salam Fayadh aliyejiuzulu mwezi Aprili, tarehe sita mwezi huu.

No comments: