Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

Hakuna mabadiliko mpaka wa Kenya na Ethiopia

Kamati ya pamoja ya uchunguzi wa mipaka ya pamoja ya Ethiopia na Kenya imetangaza kuwa, hakuna mabadiliko yoyote katika mpaka wa pamoja wa nchi mbili hizo. Ripoti ya kamati hiyo imetolewa baada ya kukamilisha kazi ya upitiaji mipaka ya pamoja ya Kenya na Ethiopia na kusisitiza kwamba, mipaka ya nchi mbili hizo iko vile vile kwa mujibu wa makubaliano ya uchoraji mipaka yaliyofikiwa na nchi hizo mbili mwaka 1970.
Kamati ya pamoja ya ufundi ya kuchungumza mipaka ya Ethiopia na Kenya iliyoanza kazi yake Mei 21 mwaka huu inajumuisha  wataalamu wa masuala ya jiografia, wataalamu wa mipaka ya kimataifa pamoja na washauri wa Wizara za Mashauri ya Kigeni wa nchi mbili hizo walikuwa na jukumu la kupitia na kuchunguza mipaka hiyo na kuibadilisha endapo wangekuta kuna mabadiliko yoyote yale katika mipaka hiyo ambayo yanakinzana na makubaliano ya mipaka ya mwaka 1970 yaliyofikiwa kati ya nchi mbili hizo. Kenya na Ethiopia zina mpaka wa pamoja wenye urefu wa kilomita 779.

No comments: