Watu 37 wameripotiwa kufariki dunia katika Jamhuri ya Afrika ya Kati
baada ya kufunikwa na mgodi wa madini. Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya
Afrika ya Kati imetangaza kuwa, tukio hilo la kuporomoka mgodi wa madini
ya dhahabu limetokea kilomita 440 mashariki mwa mji mkuu wa nchi hiyo
Bangui na kwamba, kwa akali watu 37 wameripotiwa kupoteza maisha yao
huku idadi nyingine kubwa ya watu wakijeruhiwa. Taarifa za awali
zinasema kuwa, mvua kubwa iliyofuatiwa na mafuriko ndiyo iliyosababisha
kuporomoka kwa mgodi huo wa madini.
Taarifa zaidi zinasema kuwa, kazi ya
uokozi inaendelea kwa ajili ya kujaribu kuokoa maisha ya wafanyakazi wa
mgodi huo wa madini ambao wamefukiwa na kifusi cha udongo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment