Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

Amir mpya wa Qatar kumteua Waziri Mkuu mpya

Siku moja baada ya kutwaa rasmi madaraka ya nchi, Amir mpya wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad al-Thani anatarajiwa kumteua Waziri Mkuu mpya atakayekuwa na dhima ya kuunda serikali mpya ya nchi hiyo. Duru zimefichua kwamba, Amir mpya huenda akamteua Waziri wa sasa wa Mambo ya Ndani, Sheikh Abdullah bin Nasser bin Khalifa al-Thani kuwa Waziri Mkuu mpya.
Waziri Mkuu wa sasa, Sheikh Hamad bin Jassim al-Thani amesema yuko tayari kuachia ngazi ili vijana waingie madarakani na kulisukuma mbele gurudumu la taifa. Hapo jana, Sheikh Hamad bin Khalifa al-Thani alitangaza rasmi kustaafu na kukabidhi rasmi madaraka ya nchi kwa mwanaye. Mfumo wa utawala nchini Qatar ni ule wa kifalme ambapo familia ya Aal Thani ndiyo yenye kutawala nchi hiyo. Nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi ni muitifaki wa karibu wa Marekani na katika miaka ya hivi karibuni imekuwa ikiunga mkono magaidi wanaopigana na serikali nchini Syria sambamba na kuwapa misaada ya fedha na silaha magaidi hao.

No comments: