Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 26, 2013

"Wanaosambaza silaha Syria ni maadui wa amani"

Mjumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu katika mgogoro wa Syria, al-Akhdhar Brahimi amesema wale wanaoendelea kusambaza silaha nchini Syria ndio wachochezi wakubwa wa mgogoro uliko nchini humo. Mwanadiplomasia huyo amesema kuwa, mgogoro wa Syria utakwisha punde nchi mbalimbali zitakapokoma kusambaza silaha kwa pande zinazohasimiana.
Brahim aidha ameelezea hofu yake kuhusu mazungumzo yajayo huko Geneva akisema Marekani na Russia bado hazijaonyesha irada thabiti ya kisiasa ya kusimamia mkutano huo. Amesema huenda mkutano huo uliopewa jina la Geneva 2 usifanyike mwezi ujao wa Julai kutokana na kuendelea kutokota mgogoro wa Syria. Hii ni katika hali ambayo, siku chache zilizopita, serikali ya Damascus ilitangaza kuwa iko tayari kushiriki mkutano huo na kuutaka upande wa pili pia kushiriki bila masharti yoyote. Weledi wa mambo wanasema hatua ya Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu ya kuendelea kuwapa silaha magaidi ndiyo sababu inayopelekea wao kuvimba kichwa na kukataa kushiriki kwenye mazungumzo yoyote ya amani na serikali ya Syria.

No comments: