Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, February 3, 2013

Waasi Sudan wasisitiza kuwepo amani Darfur

Mkuu wa harakati ya Uadilifu na Usawa ya nchini Sudan ametangaza utayarifu wake wa kufanya mazungumzo na serikali ya Sudan kwa lengo la kufikiwa makubaliano ya amani ya mjini Doha sambamba na kuimarisha usalama katika eneo hilo. Mkuu wa Harakati hiyo Muhammad Bashar amesema kuwa, wamechukua hatua hiyo kwa ajili ya kuwadhaminia amani wakazi wa jimbo hilo la Darfur na kwamba, pamoja na kwamba, makubaliano ya mjini Doha hayawezi kukidhi matakwa muhimu ya wakazi wa jimbo hilo, lakini usalama na amani ni msingi mkuu wa mahitaji ya wakazi.  

No comments: