Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, February 3, 2013

Mfalme wa Saudia aahidi kuwaua wakazi wa Qatif

Mfalme wa Saudi Arabia, amewatishia wakazi wa mji wa Qatifa wa mashariki mwa nchi hiyo kuwa, atatekeleza mauaji ya umati dhidi yao. Hayo yameandikwa na mtandao wa habari wa Afkar News ukimnukuu Saud bin Faisal mmoja wa wanafamilia ya kifalme nchini humo akielezea kuwa, wakazi wa mji huo wa Qatif wanaishi maisha sawa na wafungwa na kwamba, watakabiliwa na kifo.
Hii ni katika hali ambayo siku ya Alkhamis iliyopita Shirika la kutetea Haki za Binaadamu Human Rights Watch lilitangaza kuwa, mwaka uliopita wa 2012 serikali ya Saudia iliwatia mbaroni mamia ya wapinzani na wanaharakati wa kisiasa katika maeneo mbali mbali ya nchi kwa tuhuma za kutangaza misimamo yao ya kisiasa na kidini inayopingana na kukosoa serikali ya Riyadh. Aidha shirika hilo lilisisitiza kuwa, wengi wa watu hao waliotiwa mbaroni wamehukumiwa vifungo bila ya hatia.

No comments: