Maelfu ya wafuasi wa chama cha Kiislamu cha Sa'adat wamefanya maandamano
makubwa mjini Istanbul wakipinga uwekaji wa makombora ya Patriot nchini
Uturuki. Imedaiwa kuwa makobora hayo ni ya kulinda ardhi ya Uturuki.
Waandamanaji hao waliojawa na hasira pia wamepinga vikali kuingia nchini
humo askari wa kigeni kutoka nchi za Ulaya kwa minajili ya kusimamia
makombora hayo. Aidha waandamanaji walichoma picha za makombora hayo
huku wakitoa nara za kuilaani Marekani, madola ya Magharibi na serikali
ya Uturuki ya Recep Tayyip Erdoğan Waziri Mkuu wa nchi hiyo. Wamesema
kuwa, nchi za Ulaya zinaisukuma Uturuki kuingia katika mgogoro wa kivita
na nchi za eneo suala linalopingwa vikali na wananchi wengi wa nchi
hiyo. Wameongeza kwa kusema kuwa, hatua ya Shirika la Kijeshi la Nchi za
Magharibi NATO ya kuweka kambi 28 za kijeshi katika ardhi za Uturuki na
kuweka makombora ya Patriot ni hatua iliyowazi ya uvamizi wa shirika
hilo nchini Uturuki.
Sunday, February 3, 2013
Maandamano Istanbul kupinga NATO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment