Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 29, 2013

‘Yamkini serikali ya Misri ikaanguka kufuatia mgogoro’

Waziri wa Ulinzi Misri Jenerali Abdel Fattah al-Sissi ameonya kuwa mgogoro wa sasa wa kisiasa nchini humo yamkini ukapelekea kuanguka serikali.
Katika taarifa aliyotoa kupitia ukurasa wake wa Facebook, Jenerali al-Sissi amesema ‘hali mbaya itaibuka Misri iwapo wanasiasa watashindwa kutatua hitilafu zao na kukabiliana na mgogoro uliopo.’ Waziri wa Ulinzi wa Misri halikadhalika ameonya kuwa matatizo ya kiuchumi, kisiasa, kiusalama na kijamii ni tishio kubwa kwa uthabiti na usalama wa Misri.
Tokea Januari 25 karibu watu 52 wameauwa katika ghasia zilizoibuka katika miji kadhaa ya Misri ikiwemo mji mkuu Cairo, Alexandria, Suez na Port Said.

No comments: