Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Uwanja wa ndege wa Timbuktu wadhibitiwa

Vikosi vya nchi kavu vya Mali vikisaidiwa na vya Ufaransa  vimethibiti uwanja wa ndege wa Timbuktu na barabara zinazoelekea katika mji huo wa kihistoria. Luteni Kanali Diarran Kone Waziri wa Ulinzi wa Mali amesema leo kuwa, uwanja huo wa ndege umedhibitiwa bila makabiliano ya kijeshi. Taarifa zinasema kuwa waasi wa Mali wamekimbia katika mji huo baada ya kuchoma moto maktaba zilizokuwa na nyaraka zenye thamani kubwa za kale. Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa amesena kuwa, batalioni za Ufaransa na vikosi vya Mali vinaelekea katika maeneo ya biashara ya kale na vituo vya Kiislamu kwenye mji wa Timbuktu ambako inaaminika kuna makaburi ya watukufu  333 wa  Kiislamu ili kuimarisha usalama. Hayo yamejiri baada ya askari wa Mali na Ufaransa kuukomboa mji wa Gao ulioko mashariki mwa Timbuktu hapo jana,  suala linalohesabiwa kuwa ushindi mkubwa katika siku 17 za operesheni za kijeshi dhidi ya waasi wa kaskazini mwa Mali.

No comments: