Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Tunafuatilia utekelezwaji wa mkataba wa amani CAR

Umoja wa Afrika AU umetangaza kuwa, unafuatilia kwa karibu utekelezwaji wa mkataba wa amani uliofikiwa hivi karibuni baina ya makundi ya waasi na serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati. Ramtane Lamamra, Kamishna wa Umoja wa Afrika wa Masuala ya Amani na Usalama amesema, umoja huo unafuatilia kwa karibu utekelezwaji wa mkataba wa amani wa Libreville, Gabon baina ya makundi ya waasi na serikali ya Rais Francois Bozize wa Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Rais Bozize ataendelea kubakia madarakani hadi atakapomaliza muda wake mwaka 2016 lakini hatoruhusiwa kugombea Urais katika uchaguzi ujao. Aidha Rais Bozize anapaswa kuvunja serikali ya sasa ili kuruhusu kuundwa serikali ya mpito ambayo itakuwa ni ya umoja wa kitaifa. Kadhalika mkataba huo unataka Waziri Mkuu achaguliwe kutoka mrengo wa upinzani ambaye ataongoza serikali ya mpito hadi uchaguzi wa Bunge utakapofanyika katika kipindi cha miezi kumi na mbili ijayo. Tayari Waziri Mkuu ameshateuliwa na hivi sasa kinachosubiriwa ni kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa katika nchi hiyo.

No comments: