Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Kikwete: Kuna njama za kuzusha machafuko Tanzania

Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, kuna njama nyingi za kuzusha machafuko katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Rais Kikwete amedai kuwa, kuna watu wanaolipwa ili wachochee machafuko hayo kwa kutumia mgongo wa dini. Mbali na wanaotumia dini ambao amesema serikali yake itawadhibiti, Rais Kikwete ameonya kuwa, hatakubali uchochezi wa vurugu unaofanyika kupitia vyombo vya habari. Rais Kikwete amesema, hatalifungulia gazeti la Mwanahalisi lililofungiwa kwa tuhuma za uchochezi. Wakati Rais Kikwete anasema hayo, maeneo ya mikoa ya Morogoro, Mtwara na Dar es Salaam, hivi karibuni yaligeuka uwanja wa fujo na vurugu zilizosababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali. Aidha juzi hali ya utulivu na amani mkoani Mtwara ilitoweka baada ya baadhi ya wananchi kuendeleza mapambano na serikali wakipinga gesi asilia iliyovumbuliwa mkoani humo kusafirishwa kwenda Dar es Salaam bila kuwanufaisha wao kwanza.

No comments: