Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Umoja wa Afrika kutuma vikosi vya kijeshi nchini Mali

Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limetangaza kuwa, umoja huo unatarajiwa kutuma vikosi vya kijeshi kaskazini mwa Mali kwa ajili ya kusaidia operesheni ya kijeshi ya kupambana na makundi ya waasi. Hayo yamo katika taarifa ya Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika iliyotolewa jana katika kikao cha wakuu wa AU kinachoendelea mjini Addis Ababa, Ethiopia. Taarifa hiyo imeeleza kuwa, vikosi hivyo vitatumwa Mali katika fremu ya kwenda kuungana na vikosi vya Ufaransa na vile vya Mali katika operesheni ya kijeshi dhidi ya makundi ya waasi ya kaskazini mwa nchi hiyo. Taarifa hiyo aidha imeitaka serikali ya Mali kuandaa ramani ya njia na hivyo kuandaa mazingira ya kufanyika uchaguzi huru na wa kiadilifu katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika. Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limesisitizia udharura wa kuhifadhiwa umoja wa ardhi ya Mali na kwamba, suala hilo lina umuhimu wa aina yake.

No comments: