Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Mtu mmoja auawa katika machafuko Cairo

Mtu mwingine mmoja ameuawa katika machafuko mapya kati ya waaandamanaji wa Misri na vikosi vya polisi karibu na maidani ya at-Tahrir huko Cairo mji mkuu wa nchi hiyo.  Rais Muhammad Mursi wa Misri jana alitangaza hali ya hatari huko Port Said, Suez na Ismailia baada ya kujiri machafuko makubwa kwenye miji hiyo. Katika juhudi za kukomesha machafuko huko Misri, serikali ya nchi hiyo imeidhinisha rasimu ya sheria inayomruhusu Rais kutuma vikosi vya wanajeshi mitaani. Sheria pia inalipa jeshi la Misri haki ya kuwatia mbaroni raia. Muswada huo wa sheria unapaswa kwanza kupasishwa na bunge la nchi hiyo. Akilihutubia taifa kwa njia ya televisheni Rais Mursi amesema hali hiyo ya hatari itadumu  kwa siku 30 kuanzia jana usiku.  

No comments: