Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Machafuko yaendelea Misri, hali ya hatari yatangazwa

Vurugu na mapigano baina ya vikosi vya usalama na waandamanaji yameendelea kushuhudiwa katika baadhi ya miji ya Misri kwa siku ya tatu mtawalia. Habari kutoka Misri zinasema kuwa, miji kadhaa ya nchi hiyo ikiwemo ya Sharqia, Suez, Ismailia, Port Said na Cairo imeendelea kushuhudia machafuko. Hali katika mji wa Port Said inaonekana kuwa mbaya zaidi ambapo jana watu wengine saba walifariki dunia katika vurugu zilizougubika mji huo, vurugu ambazo zilishadidi zaidi baada ya Mahakama ya Jinai ya Misri kutoa hukumu ya kifo siku ya Jumamosi kwa watu 21 waliopatikana na hatia ya kushiriki katika ghasia za Februari mwaka jana zilizotokea kwenye uwanja wa mpira wa miguu baada ya mechi iliyozikutanisha klabu mbili za al Ahly na al Masry katika mji wa Port Said. Watu wasiopungua 72 waliuawa katika ghasia hizo.  Wakati huo huo Rais Muhammad Mursi wa Misri ametangaza hali ya hatari katika miji mitatu ya Port Said, Suez na Ismailia. Akizungumza kupitia televisheni, Mursi amesema, hali hiyo ya hatari iliyoanza jana katika miji hiyo itadumu kwa muda wa siku thelathini.

No comments: