Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, July 18, 2015

Saudia yatuma wanajeshi maalumu huko Yemen

Saudi Arabia imeripotiwa kutuma kikosi maalumu cha jeshi nchini Yemen kwa kisingizio cha kuwasindikiza baadhi ya maafisa watoro wa zamani wanaorejea nchini humo, hatua ambayo imetajwa kuwa inakiuka mamlaka ya kujitawa ya Yemen. Wanajeshi hao wa Saudi Arabia ambao idadi yao ni 50, watakuwa na jukumu la kuwasindikiza maafisa wa zamani watoro wa Yemen wanaorejea katika mji wa Aden kusini magharibi mwa Yemen, wakitokea Riyadh mji mkuu wa Saudi Arabia.
Hayo yameelezwa na tovuti ya habari ya Bawabatii. Wanajeshi hao maalumu wa Saudia wataendelea kuwa pamoja na maafisa hao wa Yemen baada ya kuwasili nchini humo. Maafisa watoro wa zamani wa Yemen watakaorejea Yemen wakitokea Riyadh, Saudi Arabia wametajwa kuwa ni Naibu Spika wa zamani wa Yemen, Mohammad Ali al Shadadi, Badr Mubarak Ba-Salma Waziri wa zamani wa Usafirishaji, Jenerali Ali al Ahmadi Mkuu wa zamani wa Usalama wa Taifa ambaye pia ni Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani na Mkuu wa zamani wa jeshi la wanamaji la Yemen.

No comments: