Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, July 18, 2015

Rais wa Burundi adai kulinda amani nchini

Akiwa katika kampeni zake za uchaguzi, Rais Pirre Nkurunziza wa Burundi amedai kwamba ndiye anayelinda na kudhamini amani nchini Burundi. Rais huyo ambaye anatuhumiwa na wapinzani kwa kuvuruga usalama na amani nchini amedai katika kampeni zake hizo za uchaguzi kwamba ndiye mtu pekee anayelinda na kudhamini amani katika nchi hiyo.
Rais Nkurunziza ambaye yuko chini ya mashinikizo na ukosolewaji mkubwa wa wapinzani na jamii ya kiraia nchini Burundi kutokana na uamuzi wake wa kugombea kwa mara ya tatu uchaguzi mkuu wa nchi hiyo jana Ijumaa alipeleka kampeni zake za uchaguzi katika mikoa miwili ya kaskazini mwa nchi hiyo ambayo siku chache zilizopita ilishuhudia mapigano kati ya askari wa serikali na wanamgambo. Akiwa huko Ndora mji ulio umbali wa kilomita 100 kutoka mji mkuu Bujumbura, Nkurunziza amedai kwamba tokea chama tawala kiingie madarakani mwaka 2005 hii ni mara ya kwanza kwa Warundi kutozungumzia suala la ukabila katika uchaguzi mkuu. Uamuzi wa Nkurunziza kutetea kiti chake cha urais katika uchaguzi mkuu uliopandwa kufanyika tarehe 21 ya mwezi huu umezua maandamano na malalamiko makubwa ya wananchi wanaosema kuwa unakinzana wazi na katiba ya nchi hiyo.

No comments: