Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, February 8, 2015

Waislamu waangamize Daesh bila msaada wa kigeni

Katibu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu Iran amesema, kukiwepo umoja baina ya nchi za Waislamu, magaidi wa kundi la kitakfiri la Daesh (ISIL) wataangamizwa pasina kuwepo haja ya uingiliaji majeshi wa kigeni katika ardhi za Waislamu. Mohsen Rezaei ameyasema hayo mjini Tehran wakati alipokutana na balozi wa Jordan nchini Iran siku ya Jumamosi. Akiashiria namna magaidi wa Daesh walivyomuua kinyama robani wa Jordan, Rezai amesema vitendo hama hivyo viitaongeza kasi ya kuangamia kundi hilo la kigaidi.
Afisa huyo mwandamizi nchini Iran amesema kuuawa kinyama robani wa Jordan mikononi mwa Daesh ni jambo ambalo liliamsha hisia za Waislamu na waliowengi duniani dhidi ya Daesh. Kwa upande wake balozi wa Jordan nchini Iran Abdullah Sulaiman Abdullah Abdulrahman ameishukuru Iran kwa kulaani mauaji ya robani huyo wa nchi yake. Ameongeza kuwa nchi za eneo hatimaye zitapata ushindi katika mapambano dhidi ya Daesh katika vita alivyovitaja kuwa vya kijeshi na kiutamaduni. Jumanne iliyopita magaidi wa Daesh walionyesha mkanda wa video wakimchoma kwa moto robani Moaz al-Kassasbeh, aliyetekwa nyara miezi miwili iliyopita na kundi hilo, suala lililozusha hasira za watu kote duniani. Baada ya kuoneshwa mkanda huo wa mauaji ya kutisha, Jordan ilitangaza wanachama wawili wa kundi la kitakfiri la al Qaeda waliokuwa wakizuiliwa katika jela za nchi hiyo. Aidha Jordan imetekelez oparesheni kadhaa dhidi ya ngome za Daesh nchini Syria.

No comments: