
Inadaiwa kuwa tangu mwaka uliopita wanamgambo wenye mafungamano na mtandao wa al Qaida walikuwa wanalidhibiti eneo kulikofanyika mashambulizi ya ndege hizo za Marekani.
Katika upande mwingine, vikosi vya Yemen vipatavyo 25 elfu vimekuwa vikiendesha oparesheni kubwa za kijeshi zenye lengo la kuwafurusha wanamgambo wenye silaha katika maeneo ya kusini mwa nchi hiyo, oparesheni ambazo zilianza tangu mwezi uliopita wa Mei.
No comments:
Post a Comment