Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Watoto wahanga wa kutumiwa vibaya kijinsia vitani

Taasisi moja ya Uingereza imetangaza kuwa watoto wadogo ni wahanga wakuu wa kutumiwa vibaya kijinsia wakati wa vita. Kikao cha siku nne cha kupambana na vitendo vya utumiaji mbaya wa kijinsia vitani ambacho kilizishirikisha nchi 100, taasisi zisizo za kiserikali na wataalamu wa kijeshi kimefanyika huko London Uingereza. Mwishoni mwa kikao hicho, washiriki wametaka kuweko uungaji mkono wa kimataifa ili kuweza kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria wale wote wanaohusika na jinai hiyo ya kuwatumia vibaya watoto wadogo kijinsia katika maeneo yanayokumbwa na vita.

Hii ni katika hali ambayo, Taasisi ya Kuwasaidia Watoto imeeleza kuwa watoto wadogo aghalabu huwa wahanga wakuu wa vitendo hivyo vilivyotajwa wakati wa vita. George Graham kutoka Taasisi ya Save The Children ameeleza kuwa, walimwengu hawapaswi kulipuuza suala hilo na kwamba wanapaswa kufahamu kuwa watoto ndio wahanga wakuu wa utumiaji mbaya wa kijinsia wakati wa kujiri vita. Mkutano huo wa London wa kupambana na vitendo vya kuwatumia vibaya kijinsia watoto wadogo katika maeneo ya vita umemalizika kwa kuchunguza njia mbalimbali za kukomesha unyanyasaji huo.  

No comments: