Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Ndege ya kijeshi ya Ukraine yatunguliwa

Wanajeshi wenye mfungamano na Russia huko Ukraine wameitungua ndege ya kijeshi huko katika mji wa Luhansk unaopatikana mashariki mwa Ukraine. Hayo yamethibitishwa na Wizara ya Ulinzi ya Ukraine. Duru za kijeshi za Ukraine zimeripoti kuwa ndege hiyo ya usafiri aina ya II-76 imetunguliwa leo na vikosi vya kujilinda vyenye mfungamano na Russia wakati ikikaribia katika uwanja wa ndege wa mji wa Luhansk.
Abiria wapatao 50 wanasadikiwa kuwa ndani ya ndege hiyo.
Wizara ya Ulinzi ya Ukraine imesema kuwa wanajeshi kadhaa wa miavuli na mhudumu mmoja wa ndege wamefariki dunia, huku ripoti nyingine zikibainisha kwamba wanajeshi zaidi ya 30 wameuawa katika tukio hilo.  

No comments: