Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, June 2, 2014

Wahanga wa mauaji ya Boko Haram waongezeka

Idadi ya wahanga wa shambulizi la jana la kundi la Boko Haram katika mpaka wa Nigeria na Cameroon, imeongezeka na kufikia watu 42. Kwa mujibu wa habari zilizothibitishwa na maafisa usalama nchini Nigeria, watu wasiopungua 42 waliuawa katika shambulizi hilo jipya lililofanywa na wanachama wa kundi hilo katika vijiji vya Kanari, Wazarde na Gula katika jimbo la Borno, la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Inaelezwa kuwa vijiji hivyo viko katika eneo la Gamboru karibu na mpaka wa nchi hiyo na Cameroon ambapo mwanzoni mwa mwezi uliopita kundi hilo lilifanya mauaji ya kutisha dhidi ya watu wasiopungua 300.

Mashuhuda wameeleza kuwa, watu wenye silaha wanaosadikiwa kuwa wanachama wa Boko Haram na ambao walikuwa katika malori yaliyokuwa yamebeba silaha na mada za miripuko walivamia vijiji hivyo na kuviteketeza kwa moto, ambapo mbali na kuua idadi kubwa ya watu, walijeruhi mamia ya wengine. Mashambulizi hayo yaliendelea kwa muda usiopungua masaa saba, na cha kushangaza ni kuwa hakuna askari yeyote wa serikali aliyefika eneo hilo. Hali hiyo imewafanya asilimia kubwa ya Wanigeria kuamini kuwa mashambulizi hayo yanafanyika kwa baraka za maafisa usalama wa nchi hiyo.

No comments: