Rais Hassan Rouhani wa Iran leo amemfanya mazungumzo na mgeni
wake Sheikh Sabah Al Ahmad Al Jaber Al Sabah Amir wa Kuwait mjini Tehran
na kusisitiza juu ya kuimarishwa mashirikiano ya pande mbili katika
nyanja zote. Baada ya kumalizika duru ya kwanza ya mazungumzo ya pande
mbili, Iran na Kuwait zilitiliana saini hati sita za makubaliano ya
pande mbili katika nyanja za usalama, ushuru wa forodha, uchukuzi wa
anga, utalii, hifadhi ya mazingira na michezo.
Wakati huohuo, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa,
suala la kuimarishwa uhusiano na Kuwait katika nyanja zote, linapewa
kipaumbele katika sera za kigeni za Iran.
Akizungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kumlaki Sheikh Sabah Al Ahmad Al Jaber Al Sabah
Amir wa Kuwait katika uwanja wa ndege wa Mehrabad mjini Tehran, Dakta
Muhammad Javad Zarif ameongeza kuwa, safari ya Amir wa Kuwait itaanza
kufungua ukurasa mpya wa kuimarishwa mashirikiano ya nchi hizo mbili.
Dakta Zarif ameeleza kuwa, safari iliyopangwa kufanyika hivi karibuni
nchini Saudi Arabia imeakhirishwa kutokana na safari hiyo kuingiliana na
ratiba za mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran ameeleza kuwa, mazungumzo ya
mara kwa mara ya nyuklia yatapelekea kufikiwa makubaliano ya mwisho na
kusisitiza kwamba nchi za Magharibi zilijaribu kutumia mbinu mbalimbali
kama vile vikwazo, mashinikizo na vitisho lakini hakuna hata mbinu moja
iliyoweza kuwafikisha kwenye malengo yao haramu, bali zinazidi kuwa
mbali na malengo yao siku hadi siku.
No comments:
Post a Comment