Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

"USA na waitifaki wanahusika na jinai za Daesh Iraq

Ali Larijani Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran yaani bunge amesema kuwa Marekani na waitifaki wake katika eneo la Mashariki ya Kati wanahusika katika jinai zinazofanywa na makundi ya Kitakfiri huko Iraq. Ali Larijani amesema madola makubwa yanatumia suala la ugaidi kama wenzo wao mkuu. Amesema kuwa makundi ya Kitakfiri ambayo yamekuwa yakiulenga ulimwengu wa Kiislamu yamechafua sura ya Waislamu.
Jeshi la Iraq linaendesha mapambano makali dhidi ya wanamgambo wa Kitakfiri waliosonga mbele katika mji wa Baaquba kaskazini mwa Baghdad mji mkuu wa Iraq. Itakumbukwa kuwa, kundi la kigaidi la Daesh wiki hii liliidhibiti miji miwili ya Tikrit na Mosul ambao ni mji wa pili kwa ukubwa wa Iraq. Naye Waziri Mkuu wa Iraq Noury al Maliki tarehe kumi mwezi huu alisema kuwa nchi yake inaendesha vita dhidi ya ugaidi na kusisitiza kuwa Baghdad kamwe haitaruhusu mji wa Mosul na mkoa wa Nainavah kuwa chini ya mwavuli wa magaidi.

No comments: