Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Umoja wa Mataifa wataka kusaidiwa wakimbizi CAR

Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa imeziomba nchi jirani na Jamhuri ya Afrika ya Kati kufungua mipaka yao ili kuwawezesha wakimbizi wa nchi hiyo kufika katika maeneo yenye amani. Adrian Eduardos msemaji wa Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa amesema kuwa taasisi hiyo inaziomba nchi zote jirani na Jamhuri ya Afrika ya Kati ikiwemo Chad, kufungua mipaka yake na kuwaruhusu kuingia katika nchi hizo wakimbizi na wale wanaotafuta hifadhi.

Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa Unicef pia umetangaza kuwa wakimbizi wengi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati walioko ndani na nje ya mipaka ya nchi hiyo ni watoto wadogo.  

No comments: