Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Magaidi 30 wa al-Qaida watiwa mbaroni Iran

Naibu Waziri wa Usalama wa Taifa wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza, kutiwa mbaroni magaidi 30 wa mtandao wa al-Qaida nchini hapa. Ali Khazai aliyasema hayo hapo jana kabla ya hotuba ya sala ya Ijumaa iliyosaliwa  mjini Mash'had, kaskazini mashariki mwa Iran na kuongeza kuwa, wanachama wa mtandao huo wa kigaidi, wametiwa mbaroni na askari wa usalama katika miezi ya hivi karibuni.
Akiashiria kwamba, tangu tukio la Septemba 11 hapo mwaka 2001 nchini Marekani, daima Wizara ya Usalama ya Iran imekuwa ikifuatilia kwa karibu nyendo za mtandao wa al-Qaida hapa nchini, Khazai ameongeza kuwa, makundi ya kigaidi hayaachi kufanya njama za kigaidi na uvurugaji wa usalama hasa katika maeneo matakatifu. Ameashiria jinai za makundi hayo likiwemo kundi la Dola la Kiislamu la Iraq na Sham kwa kifupi Daesh katika nchi za Kiislamu kama Iraq na Syria na kusema, mashambulizi ya makundi hayo yanatekelezwa kwa msaada na himaya kamili ya Marekani na utawala haramu wa Israel. Naibu Waziri wa Usalama wa Taifa wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameongeza kuwa, makundi ya kitakfiri na Daesh hayana uhasama na uadui na watu wa madhehebu ya Kishia peke yao, bali ni maadui na watu wa madhehebu ya Kisuni na kwamba mfano ulio wazi kuhusu suala hilo ni hujuma na jinai za hivi karibuni zilizofanywa na kundi hilo mjini Mosul, Iraq. Amesisitiza kuwa, Mashia kwa kushirikiana na wenzao Ahlu Sunna wal-Jamaa lazima waungane katika kukabiliana na makundi ya Kiwahabi na masalafi wa kitakfiri katika kila sehemu ya dunia.

No comments: