Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Kikao cha Rais Rouhani na vyombo vya habari

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa uchaguzi wa Rais wa tarehe 24 mwezi Khordad sawa na tarehe 14 Juni mwaka jana ulikuwa hapana kubwa ya taifa la Iran kwa wachupaji mipaka wa kigeni na wale wa ndani. Dakta Rouhani ameongeza kuwa, ujumbe wa tarehe 24 Khordad mwaka jana ulikuwa huu kwamba, taifa la Iran limechagua njia ya usawa, amani, urafiki, mapatano, kuamiliana na ulimwengu na njia ya ustawi madhubuti na wa kudumu, na kwamba njia hiyo ni ya kudumu kwa ajili ya taifa la Iran.
Rais Rouhani ameyasema hayo leo katika kikao na waandishi wa habari wa ndani na nje katika maadhimisho ya kwanza ya hamasa ya kisiasa ya Wairani katika uchaguzi wa Rais uliofanyika mwaka uliopita hapa nchini.
Rais Hassan Rouhani ameleza kuwa wananchi wa Iran waliutangazia ulimwengu katika uchaguzi huo kuwa, mashinikizo na vikwazo havitaathiri malengo makuu na matarajio yao. Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, iwapo lengo kuu la waweka vikwazo lilikuwa ni kutaka kuwatenganisha wananchi na mfumo wa Kiislamu, wananchi wa Iran walitangaza katika masanduku ya kupigia kura kuwa Mapinduzi na mfumo wa Iran ya Kiislamu kamwe haviwezi kutenganishika, na kwamba mashinikizo na vikwazo haviwezi kuathiri irada na malengo ya taifa kubwa la Iran.  

No comments: