Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, June 2, 2014

Syria yakosoa misimamo ya nchi za Magharibi

Feisal Miqdad, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Syria amezikosoa vikali baadhi ya nchi za Magharibi na Kiarabu kwa kuwazuia wananchi wa Syria wanaoishi kwenye nchi hizo, kushiriki katika zoezi la kupiga kura kwenye uchaguzi wa rais wa nchi hiyo. Feisal Miqdad ameongeza kuwa, baadhi ya nchi kama vile Ufaransa, Ubelgiji, Ujerumani na Bulgaria ambazo hujinadi kutetea misingi ya demokrasia zimewazuia Wasyria kushiriki kwenye uchaguzi huo. Ameongeza kuwa, baadhi ya nchi za Kiarabu nazo pia ziliamua kuchukua maamuzi hayohayo dhidi ya Syria ambayo yanakinzana na sheria za kimataifa kutokana na kuhofia mashinikizo kutoka Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria ameongeza kuwa, nchi hizo zimekiuka makubaliano ya mahusiano ya kidiplomasia ya 'Vienna'. Miqdad amebainisha kuwa, madai ya nchi hizo ya kutetea demokrasia na misingi ya haki za binadamu ni uwongo. Feisal al Miqdad ameikosoa serikali ya Ufaransa kutokana na misimamo yake ya kiadui na chuki dhidi ya Syria na kusisitiza kwamba, Paris imepoteza uhalali wake wa kimataifa, kwani katika uchaguzi wa Bunge la Ulaya uliofanyika tarehe 25 mwezi uliopita, chama tawala cha Ufaransa kilishindwa vibaya kwenye uchaguzi huo na wananchi wengi wa nchi hiyo wanataka yafanyike mabadiliko ya viongozi nchini humo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria ameongeza kuwa, serikali ya Damascus haiingilii mambo ya ndani ya Ufaransa, lakini Wafaransa wamekuwa na tabia ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi hiyo ya Kiarabu kwa kuwaunga mkono magaidi, ambao wanatenda jinai za kivita na kibinadamu nchini humo.

No comments: