Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, June 2, 2014

Israel yakerwa na mshikamano wa Wapalestina

Utawala wa Kizayuni wa Israel umetangaza kwamba utakata uhusiano wake na Mamlaka ya Ndani ya Palestina, baada ya kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa ya Palestina. Kiongozi mmoja wa utawala huo ghasibu ameiambia ofisi ya Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina kwamba, utawala wa Kizayuni utakata mahusiano yote na mamlaka hiyo, isipokuwa katika masuala ya kiusalama.
Hapo jana, viongozi wa Israel walitangaza kwamba, kamwe hawatatoa fursa kwa mawaziri watatu wa serikali ya umoja wa kitaifa kutoka Ghaza kuelekea Ramallah, Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kwa minajili ya kushiriki kwenye sherehe za kuapishwa.
Wakati huohuo, kiongozi mwingine wa kisiasa wa Israel amesema kuwa, utawala huo hautafanya tena mazungumzo na serikali mpya ya Palestima, kwa vile serikali hiyo inaishirikisha Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina 'Hamas'.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, Mahmoud Abbas Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amepanga kutangaza baraza la mawaziri hapo kesho, licha ya kukabiliwa na vitisho vya utawala wa Kizayuni wa Israel na Marekani. Imepangwa kuwa, Rami Hamdallah atakuwa Waziri Mkuu mpya wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Palestina.

No comments: