Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, June 2, 2014

Hizbullah: Rais wa Lebanon hatakiwi awe kibaraka

Muhammad Raad, Mkuu wa Mrengo wa Muqawama katika bunge la Lebanon unaojulikana kwa jina la al Wafaa amesisitiza kuwa, rais ajaye wa nchi hiyo hatakiwi kuwa kibaraka wa madola ya kigeni. Raad ameongeza kuwa, rais ajaye anatakiwa azingatie umoja wa kitaifa, awe na uchungu na nchi yake na pia asiamiliane na maadui kwa lengo la kuidhuru nchi. Ameashiria kuwa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah haiuungi mkono upande wowote katika kadhia ya uteuzi wa rais na badala yake anayataka makundi yote ya kisiasa kuweka kando tofauti zao na kumchagua rais kwa maslahi ya taifa.

Mkuu huyo wa mrengo wa al Wafaa katika bunge la Lebanon amefafanua kuwa hii leo taifa la Lebanon limechagua njia ya  muqawama na mapambano, kwani linajua kuwa ni muqawama ndio utakaoiwezesha Lebanon kupata heshima, kujitosheleza, na kuwa na uhuru wa kweli. Amesema, katika kulinda uhuru, haki ya kujitawala na kujitegemea, Lebanon haitakubali uingiliaji wa upande wowote wa kigeni katika masuala yake ya ndani. Amesema, Bairut itainyoshea nchi yoyote mkono wa urafiki na ushirikiano chini ya anga ya kuheshimiana. Licha ya wabunge wa Lebanon kufanya vikao vitano kwa ajili ya kumchagua rais mpya atakayechukua nafasi ya Rais Michel Suleiman aliyemaliza muda wake tarehe 24 mwezi uliopita wa Mei, lakini hadi hivi sasa hawajafikia makubaliano.

No comments: