Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

FAO: Misaada ya dharura ipelekwe nchini Somalia

Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa FAO limetaka misaada ya haraka ipelekwe nchini Somalia kwa shabaha ya kuondoa matatizo ya chakula yanayowakabili wananchi wa nchi hiyo. Shirika la FAO limesisitiza juu ya wasiwasi wa kupatikana dola milioni 18 ambazo zingeweza kutatua mahitajio ya dharura ya chakula nchini Somalia. Taarifa ya FAO iliyotolewa jana imeeleza kuwa, kutonyesha mvua na hali ya hewa kuwa mbaya kumechangia kwa kiasi kikubwa nchi hiyo kutumbukia kwenye matatizo makubwa ya chakula.
Naye Luca Alinovi Afisa wa FAO  katika nchi za Somalia na Kenya amesema kuwa, hali ya machafuko, upungufu wa mavuno na maghala ya chakula kuwa matupu katika maeneo makuu ya uzalishaji chakula ya kusini mwa Somalia, vimechangia kuongezeka bei ya mahindi kwa  asilimia 60 hadi 80 katika kipindi cha mwezi wa Aprili ikilinganishwa na mwaka jana.

No comments: