Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Mripuko wa Darajani, shuhuda asimulia alichokiona kwa macho yake

Hali ya usalama visiwani Zanzibar imeendelea kuwa tete baada ya watu wasiojulikana kuripuwa bomu nje ya msikiti wa Darajani kisiwani Unguja na kusababisha taharuki kubwa.
Mtu mmoja ameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika tukio hilo lililotokea baada ya mhadhara uliotolewa baada ya Sala ya Ishaa jana Ijumaa. Mhadhara huo ulihudhuriwa pia na masheikh kutoka mkoani Tanga na Mombasa Kenya

Polisi visiwani Zanzibar wamewataka wananchi watulie na wasubiri kauli rasmi kutoka serikalini, huku uchunguzi kuhusu wahusika wa shambulio hilo ukiwa umeanza mara moja.

No comments: