Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 29, 2013

Marekani kutuma ndege zisizo na rubani Afrika

Viongozi wa Marekani wanafikiria mpango wa kupeleka ndege zisizo na rubani huko kaskazini magharibi mwa Afrika.
Viongozi wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani wamesema kuwa, wanachunguza mahala itakapowekwa kambi ya ndege hizo katika eneo hilo. Hata hivyo viongozi hao wamebainisha kuwa, kuna uwezekano mkubwa kwa ndege hizo kuwekwa nchini Niger, nchi jirani na Mali. Viongozi hao wameeleza kuwa, iwapo mpango huo utatekelezwa, Washington itatuma wanajeshi wasiopungua 300 kwenye kambi hiyo. Viongozi hao wa Pentagon wamedai kuwa, lengo la kuwekwa ndege hizo zisizo na rubani ni kukabiliana na makundi ya kigaidi kama al Qaeda.
Wakati huohuo, jeshi la Ufaransa limetangaza kuwa, waasi wasiopungua 25 wameuawa kwenye mapigano yaliyojiri siku ya Jumapili katika mji wa Gao kaskazini mwa Mali.

No comments: