Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 3, 2013

Amir mpya wa Qatar aunga mkono upinzani Syria

Sheikh Tamim bin Hamad 
Amir mpya wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad bin Khalifa Aal Thani amesema kuwa nchi hiyo inaliunga mkono kundi kuu la upinzani la Syria linalojiiita "Baraza la Taifa la Syria." Sheikh Tamim amesema katika mkutano na wawakilishi wa kundi hilo mjini Doha kuwa mgogoro wa Syria utaendelea kupewa kipaumbele katika ajenda za siasa za nje za Qatar kama ilivyokuwa hapo awali. George Sabra, Abdulbasit Sida na Mohamed Farouk wanaodai ni wawakilishi wa wapinzani wa Syria, wamekutana pia na Khalid bin Mohammad al Attiyah, Waziri Mpya wa Mambo ya Nje wa Qatar.
Baraza eti la Taifa la Syria litafanya mkutano mjini Istanbul Uturuki hapo kesho ili kumchagua kiongozi wake huku Burhan Ghalioun, George Sabra na Louay M. Safi wakiwania nafasi hiyo.

No comments: