Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

Maelefu waandamana nchini Burkina Faso

Makumi ya maelfu ya wananchi wa Burkina Faso wamendamana katika mji mkuu Ouagadougou kupinga kura ya maoni inayoweza kumruhusu Rais Blaise Compaore kubakia madarakani kwa mara ya 5. Zephirin Diabre mtaribu wa maandamano hayo amesema kuwa, hawataki kipindi kisichokuwa na ukomo cha urais kwani Furkina Faso sio nchi ambayo kiongozi anatawala hadi pale anapokufa.

 Maandamano hayo yalikuwa ni jibu kwa maandamano yaliyofanywa mwezi uliopita na wafuasi wa rais Compaore ambao wanaunga mkono kura hiyo ya maoni. Compaore amekuwa rais wa Burkina Farso tangu mwaka 1987 baada ya kuongoza mapinduzi ya kijeshi, na ni mshirika muhimu wa Marekani na Ufaransa katika eneo la Magharibi mwa Afrika. 

No comments: