Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

Askari wa Marekani aachiwa huru na Taliban

Askari mmoja wa Marekani aliyekuwa akishikiliwa mateka nchini Afghanistan ameachiliwa huru kama sehemu ya makubaliano ya kubadilishana mateka na wanamgambo wa Taliban yaliyosimamiwa na serikali ya Qatar.   Serikali ya Marekani imesema kuwa, Bowe Bergdahl ameachiliwa huru mkabala wa kuachiliwa huru wafuasi watano muhimu wa Taliban waliokuwa wakishikiliwa katika jela ya Marekani ya Guantanamo Bay.
Askari huyo wa Marekani mwenye miaka 28 amekuwa akishikiliwa mateka na Taliban tangu mwaka 2009 na alikabidhiwa jana kwa vikosi vya Marekani karibu na mpaka wa Afghanistan na Pakistan.
Wakati huo huo wafungwa watano wa Taliban nao pia wameondoka katika jela ya Guantanamo Bay kuelekea Qatar. Watano hao wote walikuwa maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Taliban nchini Afghanistan iliyopinduliwa na Marekani mwaka 2001.

No comments: