Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

Wabunge nchini Yemen waitaka serikali ijiuzulu

Wabunge wa Yemen wametaka serikali ya nchi hiyo ijiuzulu wakisema kuwa imeshindwa kutatua matatizo muhimu yanayolalamikiwa na wananchi.  Yahya Ali al-Raee Spika wa Bunge la Yemen amesema wazi mbele ya Waziri Mkuu Mohammed Salem Basondowa kuwa serikali inapaswa kujiuzulu, na kuituhumu kuwa ni kama taasisi iliyojaa maafisa fisadi. Waziri Mkuu huyo wa Yemen pia amekosolewa vikali na baadhi ya wabunge kuwa si muaminifu na kwamba ameshindwa kutimiza wajibu wake.

Hata hivyo Waziri Mkuu wa Yemen ametupilia mbali madai ya kuhusika katika ufisadi na kuwapa changamoto wanaomtuhumu wathibitishe tuhuma hizo. Serikali ya maridhiano ya Yemen iliundwa mwaka 2011 nchini Saudi Arabia baada ya kiongozi wa wakati huo Ali Abdallah Saleh kulazimika kukabidhi madaraka kwa makamu wake kutokana na mashinikizo ya wananchi.

No comments: