Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

Bahrain yavunja misikiti na kumzawadia Papa kanisa

Katika hali ambayo utawala wa kifalme wa Bahrain hadi sasa umeshavunja misikiti 38 nchini humo kwa visingizio tofauti, Mfalme wa Bahrain amemzawadia Papa Francis wa Kanisa Katoliki, ramani ya kanisa kubwa linalotarajiwa kujengwa nchini humo. Taarifa zinasema kuwa, Hamad bin Isa Aal Khalifa, Mfalme wa ukoo wa Aal Khalifa wa Bahrain  aliitembelea Vatican na kukutana na Papa Francis, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duaniani na kujadiliana naye masuala mbalimbali kama vile amani katika Mashariki ya Kati, kuishi pamoja kwa usalama na amani wafuasi wa dini tofauti na kukabiliana na makundi yenye misimamo ya kufurutu mipaka katika dini.
Kanisa hilo linalotarajiwa kujengwa nchini Bahrain litakuwa kubwa zaidi kuwahi kujengwa katika nchi za Kiarabu. Wapinzani wa Bahrain wanasema kuwa, safari ya Mfalme wa Baharin huko Vatican ni hatua ya kimaonesho yenye lengo la kusafisha taswira ya utawala huo wa kidhulma ambao kwa miaka kadhaa unawakandamiza raia wanaoandamana kwa amani, hasa Waislamu wa Kishia wa nchi hiyo. Tangu kuanza harakati za mapinduzi za wananchi wa Bahrain mwaka 2012 hadi sasa, zaidi ya watu 150 wameshapoteza maisha yao kutokana na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa ukoo wa kifalme wa Bahrain huku mamia wakitiwa mbaroni kwa sababu tu ya kuandamana na kudai haki zao za kimsingi.

No comments: