Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Msafara wa kibinadamu wawasili Ukanda wa Gaza

Msafara wa misaada ya kibinadamu umewasili katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa na Israel, kama sehemu ya jitihada za kuvunjwa mzingiro huo uliowekwa na Tel Aviv dhidi ya eneo hilo la Palestina. Msafara huo unaoitwa 'The Miles of Smile 27' umewasili Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha Misri cha Rafah, huku ukiwa umebeba vifaa vya tiba na misaada ya kibinadamu. Rashad al Baz mwandamizi wa msafara huo amesema, wanaandamana na wanaharakati kutoka Algeria na Jordan na kwamba wamekwenda huko kutokana na furaha ya kufikiwa makubaliano ya umoja wa kitaifa ya Palestina.
Msafara huo una wanaharakati 25 na watabakia katika Ukanda wa Gaza kwa siku 3 ambapo watakutana na maafisa wa eneo hilo na kutembelea maeneo tofauti.
 Utawala wa Kizayuni wa Israel unazingira Ukanda wa Gaza tangu Juni 2007, hatua ambayo imepelekea Wapalestina wa eneo hilo kukabiliwa na matatizo makubwa na kuishi katika mazingira magumu.

No comments: